Kilimanjaro walilia sukari, yaadimika kilo sasa 2,500/-

Na Joyce Anael, Moshi WANANCHI mkoani Kilimanjaro wameiomba Serikali kuingilia kati tatizo la mfumuko wa bei ya sukari kutokana bei kupanda ghafla kutoka sh. 1,800 kwa kilo hadi kufikia sh. 2,500 kwa kilo licha ya sukari kuzalishwa kwa wingi katika kiwanda cha sukari cha TPC wilayani Moshi mkoani humo. Wananchi hao wamesema wanashagazwa na ongezeko la bei la ghafla huku …

Ikulu: JK hajababaika kutoa uamuzi suala la Jairo

JULAI 21, 2011, Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, akitumia madaraka yake ya Mamlaka ya Nidhamu ya Watumishi wa Umma, alitangaza hatua ya kumpa likizo ya malipo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishatai na Madini, Bwana David Kitundu Jairo, ili kupisha uchunguzi aliokuwa ameuagiza ufanyike dhidi yake. Bwana Luhanjo alichukua hatua ya kumsimamisha Bw. Jairo kufuatia tuhuma zilizokuwa zimeelekezwa dhidi yake …

HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA NNE WA BUNGE TAREHE 26 AGOSTI 2011

Mheshimiwa Spika, 1. Leo tumefikisha Kikao cha 56 tangu tuanze Mkutano wa Nne wa Bunge lako Tukufu tarehe 7 Juni 2011. Mkutano huu ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kujadili Mpango na Bajeti ya Serikali pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Wizara, Mikoa na Taasisi mbalimbali kwa mwaka 2011/2012. Tumejadili masuala mbalimbali na hasa ya kuiletea Nchi …

Wachezaji 20 Twiga Stars kwenda maputo

TIMU ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twigs Stars) inatarajia kuondoka Agosti 31 mwaka huu kwenda Maputo, Msumbiji kwenye michezo ya All Africa Games itakayofanyika nchini humo kuanzia Septemba 3-18 mwaka huu. Twiga Stars katika msafara wake itakuwa na jumla ya watu 20 ambapo kati yao 16 ni wachezaji na wanne ni viongozi wakiwemo Kocha Mkuu Charles Boniface …

Mkuchika awarejesha kazini madiwani waliotimuliwa Chadema

Na Janeth Mushi, Arusha WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Mkuchika ameamuru madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliofukuzwa kuendelea na vikao na kulipwa posho zao hadi mahakama itakapotoa uamuzi juu ya kufukuzwa kwao. Katika barua ya Mkuchika yenye kumbukumbu namba HA.23/235/01/06 iliyotolewa Agosti 23 na kumfikia Mkurugenzi …

Wakili aomba viongozi Chadema waonywe

Na Janeth Mushi, Arusha WAKILI wa Serikali, Edwin Kakolaki ameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha kutoa onyo kali katika kesi inayowakabili viongozi wa juu wa CHADEMA, hasa kwa washtakiwa wawili yaani mchumba wa Dk. Wilbroad Slaa, Josephine Mshumbuzi na Dadi Igogo kwa kile kutohudhuria mahakamani huku wakiwa na sababu zisizo na msingi. Kakolaki aliomba mahakama kupanga tarehe ya …