Usiku wa Mwanamke wa Kiafrika ndani ya TGNP

Usiku huu Septemba 15, 2011 ndani ya Viwanja vya TGNP linaendelea Tamasha la Kumi la Jinsia, wanaharakati wanaoshiriki Tamasha hilo wanakutana kwa pamoja kwenye hafla ya Usiku wa Mwanamke wa Kiafrika. Hapa kuna burudani na shughuli mbalimbali zinazofanywa na wanaharakati kienzi utamanduni wa Mwafrika. Zifuatazo ni picha mbalimbali ndani ya hafla hiyo;

Kamati ya Nidhamu kukutana Sept 24 kuwajadili Rage, Sendeu

KAMATI ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inatarajia kukutana tena Septemba 24 mwaka huu kwa ajili ya kusikiliza mashauri matatu dhidi ya Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Aden Rage na Ofisa Habari wa klabu ya Yanga, Louis Sendeu. Awali kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake Alfred Tibaigana ilikuwa ikutane Agosti 29 mwaka huu …

Rais Kikwete amtumia rambirambi RC wa Pwani

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Tanzania, Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Hajat Amina Mrisho kufuatia vifo vya watu 10 na wengine 19 kujeruhiwa kutokana na ajali ya barabarani iliyotokea Septemba 14, 2011 katika kijiji cha Mwindu wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani. Ajali hiyo ilitokea baada ya basi la Kampuni ya Grazia Safari’s kupinduka likitokea Songea …

“How To Pass Any Exam without Fear!”

Attention Parents… “Amazing, new book reveals… “How To Pass Any Exam without Fear!” IF you are interested in helping your child to Pass Exams without Fear this year, and get better grades quickly and easily then this is going to be the most exciting message you’ll ever read! Here’s why: There is an amazing new book called, ‘Winning the battle- …

Rais wa Comoro kuwasili leo Tanzania

Na Mwandishi Maalumu RAIS wa Comoro Dk. Ikililou Dhoinine anatarajiwa kuwasili nchini Tanzania leo Septemba 15, 2011 kufanya ziara ya kikazi. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu Dk. Dhoinine atawasili majira ya mchana na kupokelewa na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam. …

Wazamiaji wa Afrika Kusini ‘wachemsha’ washindwa kuifikia meli, waomba msaada

Waagiza Sub Marine kutoa Afrika Kusini Na Mwandishi Wetu, Zanzibar KAZI ya kuopoa miili ya watu walionasa kwenye mabaki ya Meli ya Mv. Spice Islanders lililokuwa likifanywa kwa pamoja na wazamiaji kutoka nchini Afrika ya Kusini na Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania hatimaye imeshindikana. Kwa mujibu wa taarifa ambazo mtandao huu imezipata leo toka kwa Ofisa Habari wa Jeshi …