Blogs Tanzania | News |  Michuzi ya Habari leo

 

Category archives for: Matukio Katika Picha

Membe Akutana na Mabalozi Kujadili Maandalizi ya Mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano

Meneja Mradi wa mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano kwa manufaa ya Wote (Smart Pertinership) Rosemary Jairo akitoa ufafanuzi kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao leo jijini Dar es salaam kuhusu maendeleo na maandalizi ya mkutano huo utakaohudhuriwa na wachumi, wanasayansi na viongozi mbalimbali wa serikali kutoka ndani na nje ya nchi.

Mzee Ally Kleist Sykes Azikwa Makaburi ya Kisutu Dar

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali, Rais wastaafu Alhaji Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu Dkt Salim Ahmed Salim, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kianana wakiungana na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Mzee Ally Kleist Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU, leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Mei 20, 2013

Mkutano wa Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete na Wabunge wa CCM

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, Mei 19, 2013, katika ukumbi wa jengo la White House, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.

Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Mifuko Hifadhi ya Jamii

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wadau na viongozi wa mifuko ya hifadhi ya jamii wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya Mifuko hifadhi ya ya jamii iliyofanyika mjini Dodoma.

Rais Kikwete Atembelea Kiwanda cha East Coast Oils & Fats

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akimimina mafuta ya virutubishi katika kinu cha kutengeneza mafuta ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kampeni ya kuhamaisha Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani, wakati alipotembelea Kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho ni kampuni tanzu ya MeTL kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Wanaoshihudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq (kushoto), Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan (wa pili kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL, Mohammed Dewji (Mb) (wa tatu kushoto) pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema akibadilishana mawazo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiq pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) wakati wakisubiri kuwasili kwa Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL kuhamasisha Lishe [...]

Hafla ya Ufungaji Mkutano wa Mamlaka za Maji Barani Afrika Dar

Rais  wa Umoja wa Mamlaka za Maji wa Bara la Afrika (AfWA), Duduzile Myeni (kulia ) akifafanua jambo wakati wa ufungaji wa mkutano unaohusu mamlaka hizo kwenye ukumbi wa mikutano wa Mlimani City jiji Dares Salaam. Kushoto ni Katibu  Mkuu wa  Wizara ya Maji , Christopher   Sayi  na kulia kwake ni  Rais wa  masuala ya Kisayansi na Kiufundi , Silver  Mugisha.

Ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi, Ole Medeye Mkoani Arusha

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi, Goodluck Ole Medeye ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi akiweka jiwe la msingi katika darasa lililojengwa kwa msaada wa wafadhili toka Marekani kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya Maingi ya Oldonyowas iliyopo kata ya Oldonyosambu, wilayani Arumeru, Arusha juzi.

 

 

Log in |

 

Google+