

Chief Judge wa Shindano la vipaji vya watoto na vijana wadogo la “MO Kids Got Talent”, Salma Mziray, akitoa maoni yake kwa baadhi ya washiriki walioingia semi finals za shindano hilo linalofanyika kwenye hotel ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar es Salaam. Kulia ni Jaji Neema Theobald na kushoto ni msanii wa filamu nchini Hidaya Njaidi wakiwa meza kuu.
Sehemu ya zawadi zilizotolewa kwa watoto walioshiriki kwenye usaili wa shindalo la “MO Kids Got Talent 2013” ambapo fainali zake zinafanyika leo kuanzia saa Kumi na moja jioni ndani ya Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar.
Mambo ya Sugua Gaga hayo…… Wapi Shaa….??? Kipaji hicho…!!!
Sehemu ya watoto wakionyesha vipaji vyao vya aina mbalimbali ikiwemo kucheza, kuimba na vingine kibao.
Kipaji cha mchezo wa Karate pia kilikuwepo.
Sehemu ya watoto wakisubiria kuingia kwenye chumba maalum kuonyesha vipaji vyao.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko akigawa zawadi zilizotolewa na MeTL Group pamoja na kupata picha ya kumbukumbu kwa washiriki waliojitokeza kwenye usaili wa shindano la “MO Kids Got Talent” ambapo fainali za shindano hilo zitafanyika leo kuanzia saa kumi na moja jioni kwenye Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar.




















