Upatikanaji mafuta Arusha bado ni tatizo

Wananchi wakiwa katika foleni za kununua mafuta.

Na Janeth Mushi, Arusha

TATIZO la upatikanaji wa mafuta bado limeendelea kuwa kero katika maeneo mengi jijini hapa kutokana na vituo kadhaa vinavyouza mafuta ya dizeli na petroli kufungwa kwa madai kuwa havina mafuta.

Uchunguzi uliofanywa na mtandao wa Thehabari mjini hapa katika maeneo mengi jana, ulishughudia kuwepo kwa foleni kubwa za magari yaliyokuwa yakisubiri mafuta hayo.

Katika kituo vya Mt. Meru kilichopo eneo la Philips barabara Kuu ya Arusha-Moshi na katika vituo vingine vya kampuni hiyo vilivyopo maeneo ya Mabuda barabra iendayo Wilaya ya Monduli, kumekuwa na msongamano mkubwa.

Vituo vingine vingi vikiwemo vya BP, kile cha Manjis kilichopo barabara ya Sokoine, kituo cha Oryx kilichopo eneo la Clock Tower na Njake kilichopo mtaa wa Goilondoi na kituo cha Engen, kilichopo barabara kuu ya Arusha-Moshi vyote vilikuwa vimefungwa kwa kukosa bidhaa hiyo.

Mfanyakazi mmoja wa kituo cha Manjis ambaye hakutaka jina lake kuchapishwa gazetini alidai kuwa wanatarajia kupata mafuta siku ya Jumatatu ijayo huku kituo cha Oryx kikidai kinatarajia kupata mafuta leo.

Related Post

One thought on “Upatikanaji mafuta Arusha bado ni tatizo

  1. Hi. I just noticed that your blog looks like it has a couple of code errors at the incredibly bottom of your websites page. Im not sure if everybody is getting this same error when browsing your site? Im employing a totally diverse browser than most folks, referred to as Opera, so thats what might be causing it? I just wanted to produce guaranteed you know. Thanks for posting some wonderful postings and Ill attempt to return back again with a totally different browser to check out things out!

Comments are closed.