Blogs Tanzania | News |  Michuzi ya Habari leo

 

Category archives for: Habari za Nyumbani

Serikali Yasema Asilimia 31 ya Watanzania ni Walevi

Serikali Yasema Asilimia 31 ya Watanzania ni Walevi

ASILIMIA 26.8 hadi asilimia 31.9 ya Watanzania wanatumia pombe na asilimia 27.4 kati ya hao ambao ni wanaume na wengine asilimia 13.4 ambao ni wanawake, ni walevi wa kupindukia. Bunge lilielezwa jana. Takwimu hizo zilitolewa na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambaye alisema kuwa viwango hivyo vimetokana na utafiti [...]

Hali Bado Tete Mtwara…Serikali Yawaonya Wanaochochea

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel NchimbiĀ 

WAKATI mtu mwingine akiripotiwa kufa, hali bado ni tete katika Mji wa Mtwara kutokana na mabomu ya machozi na risasi za moto kuendelea kurindima kwenye mitaa kadhaa wakati polisi wakipambana na makundi ya vijana wanaopinga mradi wa ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam. Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, [...]

SBL Yamtangaza Mshindi wa Mil. 1 Winda na Ushinde

Meneja wa bia ya Serengeti Allan Chonjo, akimtangaza Honest Minja (38) mshindi wa Tsh 1,000,000 wa droo ya kwanza ya Winda na Ushinde kwa wana habari katika droo iliyochezeshwa leo katika ofisi za Kampuni ya bia ya Serengeti jijini Dar es Salaam

Wakazi wa Mbezi Beach Kupima Watoto Afya ni Bure

Mkurugenzi wa hospitali ya IMTU Dkt. Ali Mzige akisitiza umuhimu wa wazazi kujali afya za watoto na kufuatilia uzito wa watoto wao walio chini ya umri wa miaka mitano alipokua akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ,Kushoto kwake ni Bw.Saibal Sarbadhikari Meneja Mkuu wa umoja wa BANGO SANGHO

Na Genofeva Matemu – MAELEZO HOSPITALI ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Tekinolojia (IMTU hospital) kwa kushirikiana na Umoja wa Jamii ya watu kutoka India Bengali waliopo nchini Tanzania watatoa huduma ya upimaji afya bure jumapili Mei 26 mwaka huu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano wanaoishi maeneo ya Mbezi Beach [...]

Nchi za Afrika zashauriwa kuwaenzi diaspora

Akitoa mada kuhusu namna Bara la Afrika lilivyoimarisha taasisi na misingi ya utawala bora, Mhadhiri kutoka Idara ya Sayansi za Siasa wa Chuo Kikuu cha Lagos, Prof. Adele Jinadu alisema katika utafiti wake kutokana na kushiriki katika tafiti tathmini kadhaa za nchi za Afrika chini ya APRM umeonesha kuwa suala la diaspora hasa haki zao za kupiga kura bado ni changamoto.

Na Hassan Abbas, Addis Ababa Viongozi wa Afrika wametakiwa kuenzi mchango wa Waafrika walioko nje ya Bara na walioko nje ya nchi zao si tu kwa kutambua mchango wao kiuchumi bali kuwapatia haki za kiraia na kisiasa ikiwemo kupiga kura. Wito huo umetolewa jijini hapa wakati wa mkutano wa siku mbili ulioandaliwa kutafakari miaka kumi [...]

Mwinyi Ataka Novemba 30 kuwa Mapumziko Afrika Mashariki

kutangaza Novemba 30 kuwa siku ya mapumziko kwa nchi zote za jumuiya hiyo ili kuongeza uelewa wa wananchi wake juu ya masuala ya mtangamano.

Na Mtuwa Salira wa EANA RAIS MSTAAFU wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi amependekeza kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kutangaza Novemba 30 kuwa siku ya mapumziko kwa nchi zote za jumuiya hiyo ili kuongeza uelewa wa wananchi wake juu ya masuala ya mtangamano. Novemba 30, 1993 ilikuwa ndiyo siku ambapo Kamisheni ya [...]

JK Alaani Vikali Vurugu za Mtwara

naamini kuwa ni jambo lisilokubalika kuwa raslimali ya nchi inaweza kuzuiliwa isitoke katika eneo ambako inapatikana kwa vile hakuna nchi yoyote duniani inayoruhusu jambo la namna hiyo. Nchi hiyo haipo na wala sera za namna hiyo haziwezi kuanzia Mtwara.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amelaani vikali fujo na ghasia zilizofanyika mjini Mtwara Jumatano, Mei 22, 2013, akisisitiza kuwa rasilimali yoyote inayopatikana katika sehemu yoyote ya nchi yetu ni mali ya Watanzania wote na lazima itumike kuwanufaisha wote. Rais anaamini kuwa ni jambo lisilokubalika kuwa raslimali ya nchi inaweza kuzuiliwa [...]

 

 

Log in |

 

Google+