Ajali feri upande wa kigamboni

Hii ndio ajali ilyotokea asubuhi hii upande wa Kigamboni ambapo gari aina ya Toyota Hilux pick up linalo tumika kusambaza nyama katika maduka ya nyama ya Kigamboni limepata ajali ya kuzama baharini baada ya kile kinachosemekana kujaribu kuwahi kuingia katika Pantoni bila mafanikio. Habari zizizo rasmi zinasema dereva wa gari amekufa na msaidizi wake amenusurika, na kwamba mwili wa marehemu umeshaopolewa lakini gari bado iko majini huku juhudi za kulitoa zikiendelea.