Blogs Tanzania | News |  Michuzi ya Habari leo

 

Mwana FA, Ommy Dimpoz kupagaisha usiku wa mtu mzima dawa

Na Mwandishi WetuWAKALI wa muziki wa kizazi kipya Mwana FA na Ommy Dimpoz wanatarajiwa kumsindikiza chipukizi mkongwe kwenye muziki wa kizazi kipya Bi Kidude kwenye maonyesho yake matatu Mkoani Mwanza. Maonyesho hayo yatafanyika kuanzia Julai sita, saba na nane, katika kumbi mbalimbali mkoani Mwanza.

Ziara hiyo imepewa jina la usiku wa mtu mzima dawa likiandaliwa na Meneja wa TMK Family, Said Fella. Fella aliliambia Blog hii kuwaonyesho la kwanza litafanyika Julai 6 (Ijumaa) katika Ukumbi wa Villa Park, jijini Mwanza.

Maonyesho mengine yatafanyika Julai 7 (Jumamosi) kwenye Ukumbi wa Ambassador Club uliyopo Geita na lile onesho la mwisho litakuwa Jumapili ya Julai 8 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza. Wasanii wengine watakaokuwemo kwenye ziara hiyo ya mtu mzima dawa, itakuwa wakali wote kutoka TMK Family kama Temba, Chegge na Aslay.

Short URL: http://www.thehabari.com/?p=19316

Posted by on Jun 26 2012. Filed under Burudani. You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. You can leave a response or trackback to this entry

Leave a Reply

*

 

 

Log in |

 

Google+