<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Blogs Tanzania &#124; News &#124;  Michuzi ya Habari leo &#187; Michezo</title>
	<atom:link href="http://www.thehabari.com/category/habari-za-michezo/feed" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://www.thehabari.com</link>
	<description>Blogs Tanzania &#124; News &#124;  Michuzi ya Habari leo</description>
	<lastBuildDate>Sat, 18 May 2013 18:43:35 +0000</lastBuildDate>
	<language>en-US</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
	<generator>http://wordpress.org/?v=3.4</generator>
		<item>
		<title>Yanga Yauwa Simba, Yaichapa 2-0 Uwanja wa Taifa</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-tanzania/yanga-yauwa-simba-yaichapa-2-0-uwanja-wa-taifa</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-tanzania/yanga-yauwa-simba-yaichapa-2-0-uwanja-wa-taifa#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 18 May 2013 16:25:44 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[featured]]></category>
		<category><![CDATA[Habari za Nyumbani]]></category>
		<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32888</guid>
		<description><![CDATA[Na Mwandishi Wetu TIMU ya Yanga ya Dar es Salaam imekamilisha mchezo wake wa mwisho wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa kuibanjua Timu ya Simba magoli 2-0 bila kujali machungu ilionayo timu hiyo kwa kukosa ubingwa wa ligi hiyo kwa mwaka huu. Mchezo huo uliovuta hisia za mashabiki na wapenzi wa mpira wa miguu [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<div id="attachment_32890" class="wp-caption aligncenter" style="width: 650px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/MG_0386.jpg"><img class="size-full wp-image-32890" title="Mchezaji wa timu ya Yanga Didier Kavumbagu akikokota mpira mbele ya mchezaji wa timu ya Simba Abdallah Seseme katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam." src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/MG_0386.jpg" alt="" width="640" height="427" /></a><p class="wp-caption-text">Wachezaji wa Simba na Yanga wakiwania mpira leo katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania Bara uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.</p></div>
<div id="attachment_32889" class="wp-caption aligncenter" style="width: 650px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/MG_0398.jpg"><img class="size-full wp-image-32889" title="Wachezaji wa timu ya Simba na Yanga wakiwania mpira wakati wa mchezo wao unaofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii." src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/MG_0398.jpg" alt="" width="640" height="427" /></a><p class="wp-caption-text">&#8216;Gooooooooo&#8230;.oooooooh&#8217;.  Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia goli baada ya kupachika mpira nyavuni leo. Golini ni Kaseja akiwa hana la kufanya baada ya mpira kutinga wavuni. (Picha kwa hisani ya FullShangwe Blog).                                 </p></div>
<p><strong>Na Mwandishi Wetu</strong></p>
<p><strong>TIMU</strong> ya Yanga ya Dar es Salaam imekamilisha mchezo wake wa mwisho wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa kuibanjua Timu ya Simba magoli 2-0 bila kujali machungu ilionayo timu hiyo kwa kukosa ubingwa wa ligi hiyo kwa mwaka huu.</p>
<p>Mchezo huo uliovuta hisia za mashabiki na wapenzi wa mpira wa miguu kwa kiasi kikubwa leo umehudhuriwa na idadi kubwa ya watazamaji, ambapo inakadiriwa kuingiza zaidi ya watazamaji 60,000 walioingia kuzishuhudia timu hizo.</p>
<p>Yanga ndiyo waliokuwa na bahati ya mapema katika mchezo huo ya kupata goli, kwani iliwachukua dakika 4 tu tangu kuanza kwa mchezo huo kabla ya kujipatia bao la kwanza, mfungaji akiwa Kavumbagu aliyepokea pasi kutoka kwa Simon Msuva.</p>
<p>Katika dakika 18 Simba ilipata penati baada ya mchezaji wa Yanga Canavaro kumuangusha mchezaji hatari wa Simba Mrisho Ngassa eneo hatari, lakini kama waswahili wasemavyo siku ya kufa nyani miti yote uteleza, Musa Mudde alikosa penati hiyo.</p>
<p>Yanga ilifanikiwa kujipatia bao la pili katika dakika 62 ambapo Hamis Kiiza alipachika bao hilo baada ya kumfikia mpira wa kurushwa toka kwa mchezaji mwenzake, Mbuyu Twite.</p>
<p>Yanga ambao walikuwa tayari wametangaza ubingwa tangu awali kabla ya michezo yake ya mwisho, imekabidhiwa kikombe chake cha Ubingwa wa Ligi Kuu wa mwaka huu pamoja na kitita cha sh milioni 70. Hadi dakika 90 za mchezo huo zikimalizika Yanga 2 na Simba 0.</p>
<p>Simba katika mchezo huo iliwakilishwa na Juma Kaseja, Nassoro Masoud, Shamte Ramadhan, Shomari Kapombe, Musa Mudde, William Lucian, Mwinyi Kazimoto, Abdallah Seseme, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba na Haruna Chanongo.</p>
<p>Yanga: Ally Mustafa, Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub, Kelvin Yondan, Athuman Idd, Simon Msuva, Franka Damayo, Didier Kavumbagu, Hamis Kiiza na Haruna Niyonzima.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-tanzania/yanga-yauwa-simba-yaichapa-2-0-uwanja-wa-taifa/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Pazia Ligi Kuu Vodacom Kufungwa Mei 18</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/pazia-ligi-kuu-vodacom-kufungwa-mei-18</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/pazia-ligi-kuu-vodacom-kufungwa-mei-18#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 17 May 2013 11:54:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32843</guid>
		<description><![CDATA[LIGI KUU ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu (2012/2013) inafikia tamati kesho (Mei 18 mwaka huu) kwa timu zote 14 kupambana katika viwanja saba tofauti. Mechi zote zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni. Ni jukumu la kamishna wa mechi husika kuhakikisha mchezo unaanza katika muda uliopangwa, vinginevyo hatua za kinidhamu zitachukuliwa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Boni-Wambura1.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Boni-Wambura1.jpg" alt="" title="Boni Wambura" width="230" height="243" class="aligncenter size-full wp-image-32844" /></a></p>
<p>LIGI KUU ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu (2012/2013) inafikia tamati kesho (Mei 18 mwaka huu) kwa timu zote 14 kupambana katika viwanja saba tofauti.<br />
Mechi zote zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni. Ni jukumu la kamishna wa mechi husika kuhakikisha mchezo unaanza katika muda uliopangwa, vinginevyo hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom toleo la 2012.<br />
Yanga ambayo tayari imeshatwaa ubingwa itakuwa mgeni wa Simba katika mechi namba 180 itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo mwamuzi atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro na Kamishna ni Emmanuel Kavenga wa Mbeya.</p>
<p>Mgambo Shooting vs African Lyon (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Mwamuzi ni Amon Paul wa Mara wakati Kamishna ni Ally Mkomwa kutoka Pwani), JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar (Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam. Mwamuzi ni Israel Mujuni wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Salum Kikwamba kutoka Kilimanjaro).</p>
<p>Tanzania Prisons vs Kagera Sugar (Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Mwamuzi ni Ibrahim Kidiwa wa Tanga wakati Kamishna ni John Kiteve kutoka Iringa), Oljoro JKT vs Azam (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha. Mwamuzi ni Athuman Lazi wa Morogoro wakati Kamishna ni Juma Mgunda kutoka Tanga).</p>
<p> Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro utatumika kwa mechi kati ya Polisi Morogoro na Coastal Union ya Tanga ambapo Mwamuzi atakuwa Said Ndege wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Hakim Byemba kutoka Dodoma. Toto Africans itacheza na Ruvu Shooting katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ambapo mwamuzi ni Geoffrey Tumaini kutoka Dar es Salaam na Kamishna ni Josephat Magazi wa Singida.</p>
<p> MECHI ZA MARUDIANO RCL WIKIENDI HII</p>
<p>Mechi za marudiano za raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zinachezwa wikiendi hii katika viwanja kumi tofauti wakati mechi ya Flamingo ya Arusha na Machava FC ya Kilimanjaro yenyewe itachezwa Jumatatu (Mei 20 mwaka huu).<br />
Uamuzi wa mechi hiyo kuchezwa Jumatatu ni kutokana na Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid kutumika kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kesho wakati Jumapili utatumika kwa shughuli nyingine za kijamii kwa mujibu wa wamiliki wa uwanja huo (CCM Mkoa wa Arusha).</p>
<p>Mechi nyingine zitachezwa keshokutwa (Jumapili) ambapo Abajalo watakuwa wenyeji wa Red Coast kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam. Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara utatumika kwa mechi kati ya wenyeji Coast United na Kariakoo ya Lindi.</p>
<p>African Sports ya Tanga itaoneshana kazi na Techfort ya Ifakara mkoani Morogoro katika mchezo utakaochezwa Uwanja wa Mkwakwani. Nayo Simiyu United ya Simiyu itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua, mjini Singida.</p>
<p>Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ndiyo utakaotumika kuzikutanisha timu za Polisi Jamii Bunda kutoka Mara na wenyeji UDC wakati Biharamulo FC ya Kagera na Polisi SC ya Geita zitaumana kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.</p>
<p>Milambo FC ya Tabora itakuwa mwenyeji wa Saigon FC ya Kigoma kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora huku Mbinga United ya Ruvuma ikiikaribisha Njombe Mji ya Njombe kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea. </p>
<p>Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa utatumika kwa mechi kati ya wenyeji 841 KJ dhidi ya Kimondo SC kutoka Mbeya. Nazo Rukwa United na Katavi Warriors zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga.</p>
<p>Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya pili zitacheza mechi zao za kwanza kati ya Mei 25 na 26 mwaka huu wakati mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.</p>
<p>UTARATIBU WA SAFARI MECHI YA TAIFA STARS v MOROCCO</p>
<p>Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litasaidia upatikanaji wa visa kwa waandishi wa habari na Watanzania wengine wanaotaka kwenda Morocco kushuhudia mechi kati ya Taifa Stars na Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.</p>
<p>Kwa ambao wangependa kupata visa kupitia TFF wanatakiwa kuwasilisha pasipoti zao, ada ya visa ambayo ni dola 50 za Marekani pamoja na picha mbili zenye kivuli (background) ya rangi nyeupe kabla ya saa 6 kamili Mei 20 mwaka huu.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/pazia-ligi-kuu-vodacom-kufungwa-mei-18/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Taifa Stars Yajiondoa Michuano ya COSAFA</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/taifa-stars-yajiondoa-michuano-ya-cosafa</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/taifa-stars-yajiondoa-michuano-ya-cosafa#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 17 May 2013 04:38:38 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32796</guid>
		<description><![CDATA[TANZANIA (Taifa Stars) imejitoa kwenye michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika nchini Zambia kuanzia Julai 2-26 mwaka huu.   Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah amesema Stars ambayo iliingizwa katika michuano hiyo kama timu mwalikwa imejitoa kutokana na mwingiliano wa ratiba [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<div id="attachment_32797" class="wp-caption aligncenter" style="width: 340px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Katibu-Mkuu-wa-Shirikisho-la-Mpira-wa-Miguu-Tanzania-TFF-Angetile-Osiah.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Katibu-Mkuu-wa-Shirikisho-la-Mpira-wa-Miguu-Tanzania-TFF-Angetile-Osiah.jpg" alt="" title="Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah" width="330" height="394" class="size-full wp-image-32797" /></a><p class="wp-caption-text">Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah</p></div>
<p><strong>TANZANIA</strong> (Taifa Stars) imejitoa kwenye michuano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Kusini mwa Afrika (COSAFA) itakayofanyika nchini Zambia kuanzia Julai 2-26 mwaka huu.<br />
 <br />
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah amesema Stars ambayo iliingizwa katika michuano hiyo kama timu mwalikwa imejitoa kutokana na mwingiliano wa ratiba kati ya michuano hiyo na mechi za Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN).<br />
 <br />
Amesema awali Tanzania ilithibitisha kushiriki michuano kwa matarajio kwamba Uganda ingekubali ombi la TFF la kubadilisha ratiba ya mechi za CHAN, lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Uganda (FUFA) likagoma kwa vile kipindi ambacho kilipendekezwa lenyewe litakuwa na uchaguzi wa viongozi wao.<br />
 <br />
Taifa Stars itacheza na Uganda (The Cranes) katika mechi za CHAN ambapo mechi ya kwanza itachezwa jijini Dar es Salaam kati ya Julai 12-14 mwaka huu wakati ya marudiano itafanyika jijini Kampala kati ya Julai 26-28 mwaka huu.<br />
 <br />
Akizungumzia michuano ya COSAFA, Kocha Kim amesema angependa kushiriki michuano hiyo kwani ingekuwa kipimo kizuri kwa kikosi chake, lakini kwa sasa malengo makubwa ya Stars kwenye mechi za mchujo za Kombe la Dunia na michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) ambayo fainali zake zitafanyika mwaka 2015.</p>
<p> <br />
<strong>TIKETI SIMBA, YANGA KUANZA KUUZWA KESHO</strong></p>
<p>TIKETI kwa ajili ya pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Yanga litakalochezwa keshokutwa (Jumamosi) kwenye Uwanja wa Taifa zitaanza kuuzwa kesho (Ijumaa) kwenye vituo mbalimbali jijini Dar es Salaam.<br />
 <br />
Vituo vitakavyouza tiketi hizo kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 10 jioni ni Uwanja wa Taifa, mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, OilCom Ubungo, kituo cha mafuta Buguruni, BMM Barbershop Sinza Madukani, Dar Live Mbagala na Sokoni Kariakoo.<br />
 <br />
Tiketi hizo zitakuwa zikiuzwa katika magari maalumu yaliyoegeshwa katika vituo hivyo. Viingilio katika mechi hiyo ya kufunga msimu ni sh. 5,000 kwa viti vya kijani, sh. 7,000 viti vya bluu, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 VIP C, sh. 20,000 VIP B n ash. 30,000 kwa VIP A.<br />
 <br />
<strong>Imeandaliwa na Boniface Wambura, Ofisa Habari<br />
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)</strong></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/taifa-stars-yajiondoa-michuano-ya-cosafa/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kocha Kim Awataja Wachezaji 26 Watakao Ivaa Morocco</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kocha-kim-awataja-wachezaji-26-watakao-ivaa-morocco</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kocha-kim-awataja-wachezaji-26-watakao-ivaa-morocco#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 17 May 2013 04:24:28 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32793</guid>
		<description><![CDATA[KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen Mei 16 mwaka huu ametaja kikosi cha wachezaji 26 watakaoingia kambini kujiwinda kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.   Katika kikosi hicho, Kim ameita wachezaji wapya sita ingawa baadhi yao wamewahi kuchezea timu hiyo, huku [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<div id="attachment_32794" class="wp-caption aligncenter" style="width: 293px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Kim-Poulsen.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Kim-Poulsen.jpg" alt="" title="Kocha Kim Poulsen" width="283" height="354" class="size-full wp-image-32794" /></a><p class="wp-caption-text">Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen</p></div>
<p><strong>KOCHA</strong> Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen Mei 16 mwaka huu ametaja kikosi cha wachezaji 26 watakaoingia kambini kujiwinda kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.<br />
 <br />
Katika kikosi hicho, Kim ameita wachezaji wapya sita ingawa baadhi yao wamewahi kuchezea timu hiyo, huku akiacha wengine watatu aliokuwa nao kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Morocco ambapo Taifa Stars ilishinda mabao 3-1.<br />
 <br />
Wapya aliowaita katika kikosi hicho kitakachoingia kambini Mei 20 mwaka huu, saa 1 jioni kwenye hoteli ya Tansoma jijini Dar es Salaam ni Ally Mustafa, Vicent Barnabas, Juma Luzio, Haruna Chanongo, Mudhathiri Yahya na Zahoro Pazi. Wachezaji aliowaacha ni Shabani Nditi, Nassoro Masoud Cholo na Issa Rashid.<br />
 <br />
Kikosi kamili cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ambacho kabla ya kwenda Morocco kitapita jijini Addis Ababa, Ethiopia kucheza mechi ya kirafiki Juni 2 mwaka huu dhidi ya Sudan ni kama ifuatavyo;<br />
 <br />
Makipa ni nahodha Juma Kaseja (Simba), Aishi Manula (Azam), Ally Mustafa (Yanga) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Shomari Kapombe (Simba), Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar) na Waziri Salum (Azam).<br />
 <br />
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Athuman Idd (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Mwinyi Kazimoto (Simba), Mudathiri Yahya (Azam) na Salum Abubakar (Azam).<br />
 <br />
Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Juma Luzio (Mtibwa Sugar), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC) na Zahoro Pazi (JKT Ruvu).<br />
 <br />
Kocha Kim amesema kikosi kitakachoingia kambini kitakuwa na wachezaji 24 ambapo Samata na Ulimwengu watajiunga na timu jijini Marrakech, lakini wachezaji atakaondoka nao Dar es Salaam kwenda Addis Ababa ni 22 ambapo ataacha kipa mmoja na mchezaji mmoja wa ndani.<br />
 <br />
Awali TFF ilikuwa imeitafutia Taifa Stars mechi ya kirafiki Juni 1 mwaka huu dhidi ya Algeria, Libya au Misri. Lakini baadaye Algeria ikasema itacheza na Togo, wakati Misri ilitaka mechi hiyo ichezwe Juni 4 jijini Cairo, jambo ambalo lisingewezekana kwa Stars kwani ina mechi ya mashindano Juni 8 mwaka huu.<br />
 <br />
Kwa upande wa Libya mechi hiyo ilikubaliwa ichezwe Tunis, Tunisia, Juni 2 mwaka huu. Lakini baadaye Libya ikataka mechi hiyo ichezewe jijini Tripoli ambapo TFF ilikataa kutokana na sababu za kiusalama.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kocha-kim-awataja-wachezaji-26-watakao-ivaa-morocco/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kiingilio Mechi ya Simba na Yanga 5,000/-</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kiingilio-mechi-ya-simba-na-yanga-5000</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kiingilio-mechi-ya-simba-na-yanga-5000#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 15 May 2013 04:57:26 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32722</guid>
		<description><![CDATA[KIINGILIO cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 18 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648. Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<div id="attachment_32725" class="wp-caption aligncenter" style="width: 500px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Nembo-ya-Timu-ya-Yanga.jpg"><img class="size-full wp-image-32725" title="Nembo ya Timu ya Yanga" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Nembo-ya-Timu-ya-Yanga.jpg" alt="" width="490" height="480" /></a><p class="wp-caption-text">Nembo ya Timu ya Yanga</p></div>
<div id="attachment_32726" class="wp-caption aligncenter" style="width: 460px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Nembo-ya-Simba.jpg"><img class="size-full wp-image-32726" title="Nembo ya Simba" src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Nembo-ya-Simba.jpg" alt="" width="450" height="429" /></a><p class="wp-caption-text">Nembo ya Simba</p></div>
<p><strong>KIINGILIO</strong> cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 18 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.</p>
<p>Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000. Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.</p>
<p>Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro ambapo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro. Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.<br />
Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.</p>
<p><strong>KOCHA KIM KUZUNGUMZIA MECHI YA MOROCCO</strong></p>
<p>Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya tiketi kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco. Mkutano huo utafanyika keshokutwa (Mei 16 mwaka huu) saa 5 kamili kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu kwenye jiji la Marrakech nchini Morocco. Taifa Stars ilishinda mechi yake iliyopita jijini Dar es Salaa kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Morocco.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kiingilio-mechi-ya-simba-na-yanga-5000/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>TFF na Ufafanuzi wa Ligi ya Mabingwa Mikoa (RCL)</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-na-ufafanuzi-wa-ligi-ya-mabingwa-mikoa-rcl</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-na-ufafanuzi-wa-ligi-ya-mabingwa-mikoa-rcl#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 15 May 2013 04:51:40 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32721</guid>
		<description><![CDATA[LIGI ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) ilianza tarehe 12 Mei 2013 ikishirikisha klabu bingwa za mikoa yote ya Tanzania Bara, isipokuwa mikoa ya Pwani na Manyara ambayo kutokana na sababu tofauti ilishindwa kuwasilisha majina ya klabu zake hadi siku ya mwisho iliyowekwa na Kamati ya Mashindano, yaani tarehe 10 Mei 2013.   Suala la kukosekana [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<div id="attachment_32723" class="wp-caption aligncenter" style="width: 340px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Angetile-Osiah1.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Angetile-Osiah1.jpg" alt="" title="Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah" width="330" height="394" class="size-full wp-image-32723" /></a><p class="wp-caption-text">Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah</p></div>
<p><strong>LIGI</strong> ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) ilianza tarehe 12 Mei 2013 ikishirikisha klabu bingwa za mikoa yote ya Tanzania Bara, isipokuwa mikoa ya Pwani na Manyara ambayo kutokana na sababu tofauti ilishindwa kuwasilisha majina ya klabu zake hadi siku ya mwisho iliyowekwa na Kamati ya Mashindano, yaani tarehe 10 Mei 2013.<br />
 <br />
Suala la kukosekana kwa wawakilishi wa mikoa hiyo miwili limezua maswali mengi kiasi kwamba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linalazimika kutoa ufafanuzi kwa faida ya wadau wote wa mpira wa miguu.<br />
 <br />
Ligi ya Mabingwa wa Mikoa, ambayo ni mpya baada ya TFF kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa mpira wa miguu, ilipangwa kuanza tarehe 5 Mei 2013, lakini hadi tarehe ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, yaani tarehe 2 Mei 2013 mikoa michache ndiyo iliyokuwa imemaliza ligi zao na kupata mabingwa.<br />
 <br />
Kuchelewa huko kwa mikoa kumaliza ligi zao kuliilazimisha Kamati ya Mashindano ya TFF kuongeza muda wa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi hao hadi tarehe 10 Mei 2013 na hivyo siku ya kuanza kwa Ligi kusogezwa mbele hadi tarehe 12 Mei 2013.<br />
 <br />
Hadi kufikia tarehe hiyo mpya ya mwisho ya kuwasilisha majina ya mabingwa wa mikoa, ni mikoa sita tu iliyofaidika na kuongezwa huko kwa muda na kupata wawakilishi wake. Mikoa hiyo ni Iringa, ambayo pamoja na kuongezwa kwa muda, iliandika barua ya kuihakikishia Kamati ya Mashindano kuwa itapata bingwa kabla ya kuisha kwa siku ya tarehe 10 Mei 2013.<br />
 <br />
<strong>Mikoa mingine ni Lindi, Mtwara, Geita, Tabora na Dodoma.</strong><br />
Mkoa wa Manyara haukuweza kumaliza ligi yake hadi mwisho wa siku ya tarehe 10 Mei 2013 na hivyo Kamati ya Mashindano iliyosubiri majina hadi saa 12:00 jioni siku hiyo kuamua kuwaondoa wawakilishi wa Manyara kwenye ratiba.<br />
 <br />
Awali, Kamati ya Mashindano iliamua kuwa ratiba ya mechi za Ligi ya Mabingwa wa Mikoa ipangwe tarehe 7 Mei 2013, ikishirikisha mikoa ambayo ilishapata mabingwa wake, lakini baada ya kuona baadhi ya mikoa ilikuwa haijakamilisha ligi zake, Kamati iliamua kuwa ratiba ipangwe kwa kutumia majina ya mikoa kwa matumaini kuwa hadi kufikia tarehe 10 Mei 2013, mikoa itakuwa imeshapata wawakilishi wake na kwa kuwa ratiba inahusu mikoa jirani, ingekuwa rahisi kwa timu kusafiri kutoka kituo kimoja hadi kingine. Lakini Mkoa wa Manyara haukuweza kufanya hivyo na Kamati kulazimika kuuondoa kwenye ratiba kutokana na kushindwa kukidhi utashi huo.</p>
<p>Mkoa mwingine ambao uliondolewa kwenye ratiba ni Pwani ambayo pamoja na kutuma jina la mwakilishi wake, Kamati ilipokea malalamiko kutoka klabu zilizoshiriki Ligi ya Mkoa, zikidai kuwa jina la bingwa wa Pwani lililowasilishwa TFF lilikuwa batili kwa kuwa klabu ya Kiluvia United haikustahili kushiriki Ligi ya Mkoa kutokana na ukweli kuwa haijasajiliwa mkoani Pwani na wala haikushiriki ligi ya mkoa msimu uliopita. Kamati ya Mashindano iliiondoa Pwani kwenye ratiba na kulirudisha suala hilo mkoani.<br />
 <br />
Ingawa Katibu wa Pwani alijaribu kuishawishi Sekretarieti ya TFF iliangalie suala hilo kwa undani zaidi, Sekretarieti ilimjibu kuwa lilishafanyiwa uamuzi na Kamati, hivyo uamuzi huo usingeweza kutenguliwa na kumshauri katibu huyo arejee mkoani kwake kuwasiliana na viongozi wenzake kuona ni jinsi gani mkoa unaweza kunusuru hali hiyo kwa kufanya uamuzi ambao ungeuwezesha mkoa kupata mwakilishi.<br />
 <br />
Kwa mantiki hiyo, masuala ya Manyara na Pwani yalikuwa ndani ya uongozi wa mikoa husika na si Kamati ya Mashindano ya TFF kwa kuwa Kamati ilitaka ipatiwe jina la bingwa ambaye alipatikana kwa mujibu wa mfumo mpya wa Ligi ya Mikoa.<br />
 <br />
Ligi ya Mabingwa wa Mikoa inachezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na hivyo timu zilizokutana tarehe 12 Mei 2013, zitarudiana mwishoni mwa wiki hii na kupatikana timu zitakazosonga mbele kwenye raundi nyingine hadi timu tatu bora zitakazopanda daraja kwenda Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zitakapopatikana. Ligi za Mikoa, kwa mujibu wa kanuni mpya, zinatakiwa ziwe na timu kati ya 16 na 20 na zinatakiwa zicheze mechi mbili za nyumbani na ugenini, hata kama zitakuwa zinatumia uwanja mmoja.<br />
 <br />
Uamuzi wa kubadilisha mfumo huo ulifanywa ili kuhakikisha kuwa mikoa inakuwa na na mashindano kwa mwaka mzima na hivyo kuiwezesha mikoa kujikita katika kutafuta mbinu za kupata fedha na kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu kwenye mikoa yao. Uamuzi huo pia unasaidia kupunguza mtindo wa wachezaji kuzunguka klabu tofauti katika msimu mmoja kwa kuwa wanalazimika kutulia kwenye klabu moja hadi muda wa usajili unapofika.<br />
 <br />
Pamoja na wachezaji kutulia sehemu moja kwa muda mrefu, pia walimu wanapata fursa ya kujikita vizuri kwenye programu zao kwa kuwa wanakuwa na uwezo wa kufuatilia maendeleo ya wachezaji wao.<br />
Pamoja na hayo yote, mfumo huo utasaidia kurudisha msisimko kwenye mikoa na hivyo kutoa fursa kwa vijana wengi wenye vipaji kuonekana na kuendelezwa.<br />
 <br />
TFF inatoa wito kwa viongozi wa mikoa kuanza kubuni sasa mikakati ya kuendesha ligi hizo msimu unaokuja kwa kuwa hakutakuwa na nafasi tena ya kuongeza muda kwa mikoa kuwasilisha majina ya wawakilishi wao.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-na-ufafanuzi-wa-ligi-ya-mabingwa-mikoa-rcl/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kiluvya United, Manyara Zaondolewa Ligi ya Mabingwa Mikoa</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kiluvya-united-manyara-zaondolewa-ligi-ya-mabingwa-mikoa</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kiluvya-united-manyara-zaondolewa-ligi-ya-mabingwa-mikoa#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 11 May 2013 05:23:58 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32596</guid>
		<description><![CDATA[WAKATI Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaanza kutimua vumbi Mei 12 mwaka huu, timu mbili zinakwenda moja kwa moja raundi inayofuata baada ya mabingwa wa Pwani, Kiluvya United kuondolewa na Mkoa wa Manyara kutowasilisha bingwa wake.   Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Mei 10 mwaka huu imeiondoa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><div id="attachment_32608" class="wp-caption aligncenter" style="width: 340px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Angetile-Osiah.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Angetile-Osiah.jpg" alt="" title="Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah" width="330" height="394" class="size-full wp-image-32608" /></a><p class="wp-caption-text">Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah</p></div><br />
<strong>WAKATI</strong> Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaanza kutimua vumbi Mei 12 mwaka huu, timu mbili zinakwenda moja kwa moja raundi inayofuata baada ya mabingwa wa Pwani, Kiluvya United kuondolewa na Mkoa wa Manyara kutowasilisha bingwa wake.<br />
 <br />
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Mei 10 mwaka huu imeiondoa Kiluvya United baada ya kubaini kuwa timu hiyo haikushiriki ligi ya mkoa wala wilaya msimu uliopita, hivyo kutokuwa na sifa ya kucheza Ligi ya Mkoa msimu huu.<br />
 <br />
Hivyo Friends Rangers ya Dar es Salaam iliyokuwa icheze na Kiluvya United na Mpwapwa Stars ya Dodoma iliyokuwa iwakabili mabingwa wa Manyara zinakwenda moja kwa moja raundi ya pili. Timu nyingine iliyokwenda moja kwa moja raundi ya pili itakayochezwa kati ya Mei 25 na 25 mwaka huu na mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu baada ya kupita kwenye upangaji ratiba ni mabingwa wa Shinyanga, Stand United FC.<br />
 <br />
Kamati hiyo iliyokutana chini ya uenyekiti wa Blassy Kiondo pia imeagiza viongozi wa mikoa ya Manyara na Pwani waandikiwe barua za onyo kwa kushindwa kuwasilisha majina ya mabingwa wao.<br />
 <br />
Vilevile imesisitiza viwanja vitakavyotumika kwa mechi za RCL ni vya makao makuu ya mikoa tu, isipokuwa kwa Uwanja wa CCM Mkamba ulioko Ifakara, Morogoro ambao ulishakaguliwa na TFF, hivyo kutumika kwa michuano ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu. Pia usajili unaotumika katika RCL ni ule ule wa ligi ya mkoa.<br />
 <br />
Mechi za Mei 12 mwaka huu zitakuwa kati ya Kariakoo ya Lindi dhidi ya Coast United ya Mtwara (Uwanja wa Ilulu), Techfort ya Morogoro vs African Sports ya Tanga (Uwanja wa CCM Mkamba), Machava FC ya Moshi vs Flamingo SC ya Arusha (Uwanja wa Ushirika), Simiyu United ya Simiyu vs Magic Pressure ya Singida (Uwanja wa Simiyu) na Polisi Jamii Bunda ya Mara vs UDC ya Mwanza (Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume).<br />
 <br />
Polisi SC ya Geita vs Biharamulo FC ya Kagera (Uwanja wa Geita), Saigon FC ya Kigoma vs Milambo FC ya Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika), Katavi Warriors ya Katavi vs Rukwa United ya Rukwa (Uwanja wa Katavi), Njombe Mji ya Njombe vs Mbinga United ya Ruvuma (Uwanja wa Sabasaba) na Kimondo SC ya Mbeya dhidi ya 841 KJ FC ya Iringa (Uwanja wa Sokoine, Mbeya).<br />
 <br />
Mechi kati ya Red Coast na Abajalo itachezwa Mei 13 mwaka huu Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Dar es Salaam. Mei 12 mwaka huu uwanja huo utatumika kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Azam na Mgambo Shooting.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kiluvya-united-manyara-zaondolewa-ligi-ya-mabingwa-mikoa/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kagera Sugar, Ruvu Shooting Kuumana Ligi Kuu Bara, Simba Mgambo Wavuna Mil 16</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kagera-sugar-ruvu-shooting-kuumana-ligi-kuu-bara-simba-mgambo-wavuna-mil-16</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kagera-sugar-ruvu-shooting-kuumana-ligi-kuu-bara-simba-mgambo-wavuna-mil-16#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 11 May 2013 02:12:42 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32578</guid>
		<description><![CDATA[KAGERA Sugar inaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo pekee wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) utakaofanyika Mei 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Katiba mjini Bukoba. Ingawa timu zote mbili hazipambani kutafuta ubingwa ambao tayari umetwaliwa na Yanga wala kukwepa kushuka daraja, mechi hiyo bado ni muhimu kwao katika mazingira matatu tofauti. Kwa mujibu [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<div id="attachment_32580" class="wp-caption aligncenter" style="width: 348px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Boniface-Wambura-TFF.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Boniface-Wambura-TFF.jpg" alt="" title="Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura" width="338" height="382" class="size-full wp-image-32580" /></a><p class="wp-caption-text">Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura</p></div>
<p><strong>KAGERA</strong> Sugar inaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo pekee wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) utakaofanyika Mei 11 mwaka huu kwenye Uwanja wa Katiba mjini Bukoba. Ingawa timu zote mbili hazipambani kutafuta ubingwa ambao tayari umetwaliwa na Yanga wala kukwepa kushuka daraja, mechi hiyo bado ni muhimu kwao katika mazingira matatu tofauti. </p>
<p>Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura ni kwamba; Kagera Sugar inayonolewa na kocha mkongwe kuliko wote katika VPL, Abdallah Kibaden na ikiwa na pointi 40 yenyewe inasaka moja kati ya nafasi nne za juu ambazo zina zawadi kutoka mdhamini wa ligi, lakini pia timu zinazoshika nafasi hizo za juu zinapata tiketi ya kucheza michuano ya BancABC Super 8.<br />
 <br />
Kwa upande wa Ruvu Shooting ya Kocha Charles Boniface Mkwasa yenye pointi 31 inasaka moja ya nafasi sita za juu ambazo ni fursa ya kuingia kwenye Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) ambayo inatarajiwa kuundwa baada ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Septemba 28 mwaka huu.<br />
 <br />
Wagombea nafasi za uenyekiti na makamu wake ni lazima watoke katika timu zilizoshika nafasi sita la juu katika VPL msimu uliopita. Uchaguzi wa TPL Board utafanyika siku moja kabla ya ule wa TFF uliopangwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu.<br />
 <br />
Raundi ya 25 ya ligi hiyo itakamilika keshokutwa (Mei 12 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji Azam na Mgambo Shooting ya Tanga. Mechi hiyo namba 169 itachezwa katika Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Azam yenye pointi 48 inahitaji moja zaidi ili kutetea nafasi yake ya umakamu bingwa iliyoutwaa msimu wa 2011/2013 na kupata tiketi ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.</p>
<p>Wakati Azam ikisaka pointi hiyo moja, Mgambo Shooting inayofundishwa na wachezaji wa zamani wa mabingwa wa Tanzania Bara mwaka 1988, Mohamed Kampira akisaidiwa na Joseph Lazaro ni moja ya timu ziko katika hatari ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu ujao.<br />
 <br />
Mgambo Shooting inahitaji pointi moja tu katika mechi mbili ilizobakiza kukwepa kurudi FDL, ikishindwa kupata pointi hiyo huku Polisi Morogoro na Toto Africans ya Mwanza zikishinda mechi zao za mwisho kwa uwiano mzuri wa mabao itakuwa imekwenda na maji.<br />
 <br />
Mechi ya Azam dhidi ya Mgambo Shooting itachezeshwa na refa Jacob Adongo kutoka Mara, na atasaidiwa na Abdallah Rashid wa Pwani na Charles Mbilinyi wa Mwanza. Mwamuzi wa mezani atakuwa Idd Lila wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Omari Walii wa Arusha.<br />
 <br />
<strong>SIMBA, MGAMBO SHOOTING ZAINGIZA MIL 16</strong></p>
<p>Mechi namba 149 ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Simba na Mgambo Shooting iliyochezwa juzi (Mei 8 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kushinda bao 1-0 imeingiza sh. 16,651,000.<br />
 <br />
Watazamaji 3,006 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 3,226,125 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 2,539,983.05.<br />
 <br />
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 1,640,402.54, tiketi sh. 3,175,000, gharama za mechi sh. 984,241.53, Kamati ya Ligi sh. 984,241.53, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 492,120.76 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 382,760.60.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/kagera-sugar-ruvu-shooting-kuumana-ligi-kuu-bara-simba-mgambo-wavuna-mil-16/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>TFF Yampa Siku Saba Mwandishi Dauda Kujieleza</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-yampa-siku-saba-mwandishi-dauda-kujieleza</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-yampa-siku-saba-mwandishi-dauda-kujieleza#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 11 May 2013 02:11:38 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[featured]]></category>
		<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32579</guid>
		<description><![CDATA[SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtaka Shaffih Dauda ambaye ni mmiliki wa tovuti ya www.shaffihdauda.com kutoa maelezo kuhusiana na barua ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) aliyoiweka kwenye mtandao wake huo.   FIFA ambayo ilisimamisha mchakato wa uchaguzi wa TFF baada ya baadhi ya wagombea kuulalamikia, baadaye ilitoa maelekezo kuhusu [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><div id="attachment_32581" class="wp-caption aligncenter" style="width: 338px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/TENGA1.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/TENGA1.jpg" alt="" title="Rais wa TFF, Leodger Tenga" width="328" height="356" class="size-full wp-image-32581" /></a><p class="wp-caption-text">Rais wa TFF, Leodger Tenga</p></div><br />
<strong>SHIRIKISHO</strong> la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtaka Shaffih Dauda ambaye ni mmiliki wa tovuti ya www.shaffihdauda.com kutoa maelezo kuhusiana na barua ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) aliyoiweka kwenye mtandao wake huo.<br />
 <br />
FIFA ambayo ilisimamisha mchakato wa uchaguzi wa TFF baada ya baadhi ya wagombea kuulalamikia, baadaye ilitoa maelekezo kuhusu mchakato huo kwa barua ambayo iliituma kwa Rais wa TFF, Leodegar Lenga.<br />
 <br />
Rais wa TFF katika mkutano wake na waandishi wa habari ambao Dauda alihudhuria alibainisha kuwa barua hiyo ya FIFA hawezi kupewa kila mtu, na kuruhusu waandishi kuisoma kwa Ofisa Habari wa TFF bila kuondoka nayo.<br />
 <br />
Wakati Rais Tenga anazungumza na waandishi wa habari (Mei 2 mwaka huu), nakala ya barua hiyo ya FIFA ilikuwa kwa viongozi wakuu wa TFF pekee, na viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Hivyo TFF imemtaka Dauda kutoa maelezo ya mahali alipoipata barua hiyo ndani ya siku saba.<br />
 </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-yampa-siku-saba-mwandishi-dauda-kujieleza/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>TFF Kufanya Uchaguzi Mkuu  Septemba 29.</title>
		<link>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-kufanya-chaguzi-mkuu-septemba-29</link>
		<comments>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-kufanya-chaguzi-mkuu-septemba-29#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 09 May 2013 12:46:18 +0000</pubDate>
		<dc:creator>jomushi</dc:creator>
				<category><![CDATA[Michezo]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.thehabari.com/?p=32521</guid>
		<description><![CDATA[MKUTANO MKUU wa Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unatarajiwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu baada ya ule wa Dharura wa marekebisho ya Katiba ulipangwa kufanyika Julai 13 mwaka huu. Tarehe hizo zimepangwa na kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kilichofanyika leo (Mei 9 mwaka huu) jijini Dar es [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><div id="attachment_32522" class="wp-caption aligncenter" style="width: 299px"><a href="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Copy-of-Ofisa-Habari-TFF.jpg"><img src="http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2013/05/Copy-of-Ofisa-Habari-TFF.jpg" alt="" title="Afisa habari wa TFF Boniface Wambura" width="289" height="344" class="size-full wp-image-32522" /></a><p class="wp-caption-text">Afisa habari wa TFF Boniface Wambura</p></div><br />
MKUTANO MKUU wa Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unatarajiwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu baada ya ule wa Dharura wa marekebisho ya Katiba ulipangwa kufanyika Julai 13 mwaka huu.<br />
Tarehe hizo zimepangwa na kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kilichofanyika leo (Mei 9 mwaka huu) jijini Dar es Salaam chini ya uenyekiti wa Rais wake Leodegar Tenga ambacho kupokea rasmi maagizo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na kupanga utekelezaji wake.</p>
<p>“Kamati ya Utendaji ya TFF imepokea rasmi barua ya FIFA na kupanga utekelezaji wake. Tumepokea maagizo ya FIFA yanayotuelekeza cha kufanya, si TFF wala mtu mwingine yeyote anayeweza kuongeza jambo lingine.<br />
“Maagizo ni undeni Kamati ya Maadili, Kamati ya Rufani ya Maadili, fanyeni marekebisho ya Katiba, anzeni tena uchaguzi, waliokuwepo na wengine wapya waruhusiwe. Tumejitahidi kuhakikisha uchaguzi uwe kabla ya Oktoba 30 mwaka huu kama FIFA walivyotuagiza,” amesema Rais Tenga wakati akizungumza na waandishi wa habari.</p>
<p> Amesema kazi kubwa itakuwa ni kutayarisha kanuni hizo, kwani Kamati za Maadili lazima ziwe na kanuni zake na kuhakikisha kuwa hakuna mgongano kati ya Kanuni za Nidhamu na Kanuni za Maadili.</p>
<p> Pia Rais Tenga amesema kuna kazi ya kuangalia jinsi zitakavyoingia katika uchaguzi ambapo maana yake muda wa mchakato wa uchaguzi utakuwa zaidi ya siku 40 za sasa, hivyo mabadiliko hayo yatagusa vilevile Kanuni za Uchaguzi.<br />
Kwa mujibu wa ratiba ya utekelezaji, rasmu ya mwanzo ya Kanuni hizo inatakiwa iwe imetoka kufikia Mei 30 mwaka huu ambapo itapelekwa FIFA kwa ajili ya kupata mawazo yao kabla ya kuendelea na hatua inayofuata.<br />
Juni 15 mwaka huu Kamati ya Utendaji ya TFF itakutana kupokea mapendekezo hayo ambapo baada ya kuyapitisha itayapeleka tena FIFA. Taarifa (notice) ya Mkutano Mkuu wa Dharura ambayo kikatiba ni siku 30 itatolewa Juni 12 au 13 mwaka huu.<br />
Baada ya Mkutano Mkuu wa Dharura wa marekebisho ya Katiba, Kamati ya Utendaji itakutana kati ya Julai 14 na 15 mwaka huu kuunda Kamati ya Maadili na Kamati ya Rufani ya Maadili ili kuruhusu mchakato wa uchaguzi uanze. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.thehabari.com/habari-za-michezo/tff-kufanya-chaguzi-mkuu-septemba-29/feed</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
